MAMBO YA KUZINGATIA KABLA YA KUINGIA KWENYE NDOA

By
Advertisement
NI VEMA UKAYAJUA HAYA KABLA YA KUINGIA KWENYE NDOA:


SOCIAL HALL

1. Sherehe ya Harusi ni ya siku moja tu, na Ndoa ni ya maisha yote.

2. Mwanamume/Mwanamke aliyezoea kuchepuka kabla ya Ndoa, ataendelea kuchepuka hata baada ya Ndoa.

3.Upole na ukimya si kiashiria cha tabia njema.

4. Ukikitaka ambacho hakijawahi milikiwa na mtu yeyote, ni lazima ufanye jambo ambalo halijawahi fanywa na mtu yeyote.

5. Mungu akitaka kukubariki hukuletea mtu, na Shetani akitaka kukuangamiza hukuletea mtu.

6. Bora uishi mwenyewe kuliko kuoa ama kuolewa na mtu asiye sahihi.

7. Aina tatu za wanaume wakuepukwa:
(a) Walevi
(b) Wazinzi
(c) Wagomvi.

Aina tano za wanawake wa kuepukwa;
   (a) Walevi
   (b) Wazinzi
   (c) Wachawi
   (d) Wagomvi
   (e) wasio tii

8 .Kuolewa na Mchekeshaji hakutakufanya uwe na Ndoa yenye furaha.

9. Maneno matatu yanayojenga amani katika Ndoa:
 (a) Nakupenda.
 (b) Samahani.
 (c) Asante.

10. Kupiga punyeto kwa mwanaume na kujichua kwa mwanamke ni kuharibu mwili wako mwenyewe.

11. Kuoana kabla ya kuwa marafiki ni kama gari bila mafuta. Hamuwezi kufika popote.

12. Mafanikio ya Ndoa siku zote ni pembetatu:
>Mungu mmoja
> Mume mmoja
> Mke mmoja.

13. Furaha ya kudumu maishani hutegemea na chaguo lako la mwenzi ktk Ndoa.

14. Usioe/kuolewa na pesa au mali. Oa/Olewa na mtu. Pesa/Mali hufilisika lakini utu hudumu milele.

15. Uchumba uliovunjika ni bora zaidi kuliko Ndoa isiyo na amani wala furaha.

16. Usiweke kipaumbele chako kwa muonekano mzuri wa mwanamke. Hakuna mwanamke mbaya, bali anahitaji kupendezeshwa.

17. Mapenzi si upofu. Upofu ni kuoa ama kuolewa na mwanamume/mwanamke kwa sababu tu anakidhi haja zako kingono.

18. Ukiwa rafiki mwema, utawavutia marafiki wema. Vivyo hivyo kwa marafiki wabaya (Bad company corrupt good character)

19. Asili ya mikono inayojali ni moyo unaojali.

20. Iepuke Ndoa mbaya kabla haijaanza...

""Mungu awabariki Sana"". SOCIAL HALL

0 comments:

Mr.Kikoti. Powered by Blogger.

Comments